Tuesday, September 27, 2011

PAULSEN ATANGAZA KIKOSI CHA MAUAJI DHIDI YA MOROCCO

Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Jan Poulsen leo (Septemba 27 mwaka huu) ametangaza kikosi cha wachezaji 23 kwa ajili ya mechi ya mwisho ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwakani dhidi ya Morocco.

Kikosi hicho kitaingia kambini Septemba 29 mwaka huu jijini Dar es Salaam, na kinatarajiwa kuondoka nchini Oktoba 6 mwaka huu kwenda Casablanca, Morocco kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa Oktoba 9 mwaka huu kwenye mji wa Marrakech.

Wachezaji walioitwa ni 
MAKIPA Shabani Dihile (JKT Ruvu Stars), Juma Kaseja (Simba) na Shabani Kado (Yanga). 

MABEKI WA PEMBENI ni nahodha Shadrack Nsajigwa (Yanga), Erasto Nyoni (Azam), Idrissa Rajab (Sofapaka, Kenya) na Amir Maftah (Simba). Mabeki wa kati ni Aggrey Morris (Azam), Juma Nyoso (Simba) na Victor Costa (Simba).

VIUNGO WAKABAJI ni Henry Joseph (Kongsvinger IL, Norway), Nurdin Bakari (Yanga), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar) na Jabir Aziz (Azam). Viungo washambuliaji ni Nizar Khalfan (Vancouver Whitecaps, Canada), Mrisho Ngassa (Azam) na Ramadhan Chombo (Azam).

WASHAMBULIAJI ni Abdi Kassim (DT Long An, Vietnam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Dan Mrwanda (DT Long An, Vietnam), Athuman Machupa (Vasalund IF, Sweden), John Bocco (Azam) na Hussein Javu (Mtibwa Sugar).

Athumani Machupa ,Mmoja ya washambuliaji waliomo ndani ya kikosi cha mauaji(TAIFA STARS)
ambaye anatokea VASALUND/FC KILIMANJARO Za SWEDEN.


Thursday, August 11, 2011

STHLM ALL WHITE PARTY 2011

PRESNTED BY: FREDDYNICE/GONGA
"We actually hanging out together,working together,neighbours,you know kind f down for what ever brothers,then this other day,. we decided doing entertainment business.,as in parties n styles.classy clean,fresshh u know ,.magnificent black flagging,white as we luv parties,.like trully trully luv life.

After the Stockholm White Party 2010, IceBlackMagic 2011 N SPRING BREAK 2011 feat LADY JAY DEE Pulled Off,,,This time niceGONGA again in collabolations with GREY GOOSE VODKA brings to you STHLM ALL WHITE PARTY 2011....HOTTEST PARTY OF THE SUMMER RETURNS FOR SEASON TWO.

All white attire required/Mandotory attire required.
Ladies: Classy & Sophisticated
Gentlemen: Swagger & Smooth
Side note: feel free to accesorize}green, yellow, blue, silver..

RSPV: FREDDYNICE+4673 672 4708
FRANK GONGA +255655400411

More info:www.stockholmwhiteparty.bl​ogspot.com

Thursday, August 4, 2011

OMARY NA DJ RICH WA STOCKHOLM WAFIWA NA BABA YAO MZAZI.

OMARY MSUO.
Kwa habari tulizozipata hivi punde kutoka kwa katibu wa kamati ya muda iliyopewa dhamana ya kuunda Chama rasmi cha watanzania waishio Sweden TASWE,Ndugu Adrey Yustace,,ni Kwamba Ndugu yetu Omary Msuo na mdogo wake Dj Rich wamefiwa na baba yao Mzazi.,Omary amefanikiwa kuwahi mazishi na kisomo kinatarajiwa kufanyika pindi atakaporudi,Watanzania tulioko Sweden tuungane kwa pamoja kuwafariji ndugu zetu hawa waliopo kwenye kipindi hiki kigumu.,Habari zaidi Zitawajia pindi tutakapozipata kutoka kwa wafiwa..MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU PEPONI,,AMEN.

Poulsen: Ulimwengu tafuta timu

KOCHA mkuu wa timu ya taifa ' Taifa Stars', Jan Poulsen amesema hana mpango wa kumuita mshambuliaji wa timu ya taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 23, Thomas Ulimwengu katika kikosi chake kwa sababu hana klabu.



Poulsen ametoa kauli hiyo katika kipindi ambacho taifa Stars inahitaji washambuliaji mahili kama alivyo Ulimwengu na Mbwana Samatta anayecheza katika klabu ya TP Mazembe ya DR Congo.

Akizungumza na Mwananchi jijini Dar es Salaam, Poulsen alisema mchezaji huyo yuko katika kiwango kizuri na anastahili kuchezea timu ya taifa, lakini  anavyokosa timu ya kuchezea ndiyo inayomnyima nafasi katika kikosi cha Stars.

"Thomas ni mchezaji mzuri na alionyesha kiwango kikubwa sana katika mechi mbili alizocheza jijini Arusha dhidi ya timu ya taifa ya Shelisheli na anastahili kuchezea timu ya taifa, lakini tatizo lake ni moja tu! hana timu,”alisema Poulsen.

Alisema,"Binafsi nimeshazungumza na Ulimwengu na nikamshauri kuwa hivi sasa anapaswa kutafuta timu ili aweze kuchaguliwa  timu ya taifa kwa sababu ana kiwango kizuri ingawa amekaa muda mrefu bila kucheza hivyo anakosa vitu vichache ambavyo vinaweza kuigharimu timu ya taifa kwa hivi sasa endapo atapewa nafasi."

"Na atakapopata nafasi ya kucheza timu ya taifa ndipo atakapopata pia nafasi katika timu zingine kubwa za nje kama alivyofanya Mbwana Samatta kwa sababu mchezaji mwenye kiwango kizuri kama Ulimwengu ama kama alivyokuwa Samatta anapocheza timu ya taifa hawezi kukosa timu nje ya nchi”.

Kocha huyo alitoa maelezo hayo baada ya kuulizwa juu ya  mikakati yake ya kuwatumia vijana katika kikosi kitachocheza na Algeria katika mechi ya kuwania kufuzu mashindano ya Afrika (AFCON).

Akifafanua zaidi juu ya soka la vijana alisema,"timu ya vijana chini ya miaka 23 ina wachezaji  wazuri na wote wana uwezo mkubwa kwa sababu wamekaa pamoja ingawa sifa namba moja ya mchezaji kuitwa timu ya taifa ni mchezaji huyo kuwa na klabu inayoshiriki Ligi Kuu yoyote Duniani”:

Ingawa viwango vya vijana hao ni vizuri na baadhi yao hawataweza kuendelea kuichezea timu hiyo kwa sababu ya umri wao hivyo wanapaswa kuchangamkia nafasi ya kupata timu za Ligi Kuu haraka ili waingie Taifa Stars.

Wakati Poulsen akimshambulia mshambuliaji huyo na wenzake kutafuta timu hasa ndani ya nchi, Ulimwengu kwa upande wake amesema hawezi kucheza soka la Tanzania kwa ajili ya kuingia timu ya taifa.

"Anachosema kocha ni kweli na pia ni sahihi kabisa, lakini mimi siwezi kucheza soka la Tanzania kwa ajili ya kuingia timu ya taifa, mimi nina mikakati yangu ninayoisubiri na wakati utakapofika nitaiweka wazi kwa watanzania wote,"alisema Ulimwengu.

Alisema anatambua umuhimu wa timu ya taifa, lakini pili anazingatia maisha yake ya baadaye ya soka na kwamba hiki ndicho kipindi chake cha kuandaa maisha yake ya baadaye ambayo pia yanaweza kuisaidia Taifa Stars kwa siku za usoni kuliko hivi sasa.
                                                         Zoom for better video.
Thomas Ulimwengu ni miongoni ya wachezaji mahili waliyowahi kuichezea timu ya FC KILIMANJARO ya SWEDEN.

Wednesday, August 3, 2011

Ten-man Malmö overcome nine-man Rangers

Malmö FF 1-1 Rangers FC (agg: 2-1)
In an incident-filled match, Jiloan Hamad's 80th-minute strike earned Malmö a place in Friday's play-off draw.


Ten-man Malmö FF left it late to secure a UEFA Champions League play-off berth at the expense of Rangers FC, who finished the game two players down.
Rangers' task of overturning a 1-0 deficit was made all the more difficult when Steven Whittaker received his marching orders on 19 minutes. However, Ally McCoist's men were level on aggregate soon after through Nikica Jelavić. Madjid Bougherra's 66th-minute red card gave the Swedish champions a further numerical advantage before Ricardinho's dismissal made it ten against nine. Both sides looked to exploit the extra space but it was Jiloan Hamad's wonderful volley ten minutes from time that settled the tie.
Needing to cancel out Daniel Larsson's first-leg winner, Rangers started positively, Lee Wallace testing Dušan Melichárek early on with a free-kick. McCoist's charges remained undeterred after Whittaker's straight red card and levelled the tie via Jelavić's strike five minutes later.
For all their endeavour the hosts rarely troubled Allan McGregor in the visitors' goal before the break. Rikard Norling's half-time team talk prompted an improved performance after the restart, however, and they were soon up against nine men following Bougherra's departure for a foul on substitute Dardan Rexhepi.
Malmö began to exploit the extra space and twice came close through Wílton Figueiredo but the Brazilian forward fired over the crossbar. Jelavić wasted Rangers' best chance of the half before Ricardinho received his second booking for a foul on Steven Naismith.
The hosts continued to push forward, though, and finally broke Rangers' resistance, Hamad finding space on the edge of the penalty area before unleashing an unstoppable dipping volley into the top right-hand corner. Malmö will discover their play-off opponents when the draw is made on Friday.

MASHABIKI WAMWAGIA BOBAN MAMILIONI...BIG UP HOMEBOY,,,KAMA IPO IPO TU



PAMOJA na uongozi wa Simba kumlipa mshahara wa Sh 800, 000 kwa mwezi, kiungo maestro, Haruna Moshi ‘Boban’, mashabiki wawili wa klabu hiyo wamejitolea kumuongezea fedha nyingine na kumfanya awe juu zaidi.

Ongezeko hilo la mashabiki hao wawili wa Simba linamfanya Boban ajikusanyie kitita cha karibu Sh milioni 1.9 kwa mwezi, hivyo kuwa mmoja wa wachezaji wanaolipwa zaidi katika klabu hiyo na wale wanaoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom.

Kitita hicho cha Sh milioni 1.9, kama ni kwa mwaka mzima maana yake Boban atakuwa akichukua Sh milioni 22.8 ambacho ni kiwango cha juu zaidi.
 Kila mwisho wa mwezi, mmoja wa wanachama hao humpa Boban dola 400 (zaidi ya Sh 600,000), huku mwingine akitoa Sh 500,000 hivyo kumfanya apokee jumla Sh milioni 1.9 kwa mwezi
.
Boban amerejea Simba baada ya kuvunja mkataba wake na Gefle IF ya Sweden iliyokuwa inamlipa kitita cha dola 5,000 (Sh milioni 7) kwa mwezi.
Kiungo huyo ndiye tegemeo kubwa la uchezeshaji katika kikosi hicho cha Msimbazi chini ya Kocha Mkuu, Moses Basena raia wa Uganda.

Tokea amerejea Simba ameonyesha uwezo mkubwa, hasa katika michuano ya Kagame ambayo kikosi hicho kiliingia fainali na kukutana na watani wao Yanga walioshinda kwa bao 1-0 na kutwaa ubingwa.
Katika michuano hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Boban alikuwa kati ya wachezaji waliotoa pasi nyingi za uhakika.